HomeResourcesSabbath School quarterly
Maandiko, Mamlaka
20/04/2026
Inapokuja kwa katika mafunzo binafsi ya Biblia ni lazima tuwe waangalifu tusitazamie Biblia kutimiza makusudi au maoni yetu, ambayo si wakati wote yanapelekana na ya Mungu. Kwa mfano, hatupaswi kutumia njia ya “kufunga macho yangu na kuelekeza kwenye fungu,” kwa sababu hii sivyo Mungu anataka kuwasiliana nasi kupitia Neno Lake. Mungu si kikaragosi kwenye kamba, anayesubiri kutumikia mahitaji na mapenzi yetu. Njia Zake na mawazo Yake ni ya juu sana kuliko yetu (Isa. 55:9), na hivyo tusijaribu kamwe kuthibiti maneno Yake kwetu. Wala hatupaswi kuchagua na kubagua tu sehemu za Biblia ambazo tunajisikia vizuri tunapozisoma. Badala yake, tunapaswa kuiona Biblia katika ujumla au katika ukamilifu wake badala ya kusoma vifungu rahisi, vinavyojulikana na kuacha vile vinavyotukabili au vyenye kutupatia changamoto. Ikiwa kwakweli tunataka Mungu azungumze katika maisha yetu, ni lazima tuchukue Biblia katika ujumla wake na kutumia njia zinazofaa tunaposhiriki katika mafunzo ya Biblia kwa uangalifu, tukitumaini kwamba Mungu atafunua kile tunachohitaji kusikia tunapohitaji kuisikia.
Vilevile, Bwana Yesu Mwenyewe anatuambia: “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote” (Mt. 22:37). Yaani, Mungu hataki tupuuzie mawazo yetu; badala yake, anataka kujaza akili zetu kwa wingi wa maarifa na ufahamu, ambavyo vimedhihirishwa, kwa sehemu, kupitia katika Neno Lake. Tunaweza kusoma maelezo mengi ya kibiblia ambamo Mungu alikuwa na mijadala na watu kama vile Henoko, Ibrahimu, Musa na Ayubu, ukiongezea kwa mijadala mingi ambayo Yesu aliifanya na watu. Mungu haruki mantiki za kibinadamu bali anatualika tuzisalimishe kwa Neno na hekima Yake anapotendea kazi wokovu wetu.
Hata hivyo, mantiki ya kibinadamu, bado inao uwezekano wa kuwa na makosa ya kibinadamu na udanganyifu. Kamwe haina ukamilifu. Inawezekana kulingana na mantiki ya kibinadamu kumweka Mungu pembeni kujaribu kufanya mambo peke yetu, jambo linaloweka nafsi kuwa sawa na, au juu kuliko, Mungu inapokuja katika kufikiri. Watu wanaweza kuyakabili Maandiko wakiwa na roho ya kiburi na ya ukosoaji, wakidhani kwamba wamewahi kuyajua yote kabla na kwamba hakuna jipya kwao. Ni Pale tunapojisikia kuwa wenye umuhimu sana, wenye ujasiri, kuridhika nafsi, na tukiwa hatuna hitaji la chochote ndipo tunapopuuzia uhusiano wetu na Mungu na kutegemea ujuzi wetu mdogo ulio na ukomo pamoja na mantiki zetu zenye makosa.