HomeResourcesSabbath School quarterly

Jifunze zaidi

12/06/2026

Ni wakati tunapokumbana na changamoto za maisha na tunapohitaji kushikamana na Mungu kwa nguvu zaidi. Mada tulizochunguza katika robo hii zote zinachangia kudumisha au kufufua kutembea kuliko imara pamoja na Mungu. Unapokumbana na vikwazo kama vile changamoto za kiafya, matatizo ya kifedha, kuvunjika kwa ndoa, kifo cha mtu wa karibu, au mzigo mwingine unaokuondolea furaha, tafakari maswali yafuatayo na uzingatie masomo uliyojifunza hadi sasa.

Masawali ya Kujadili

Muhtasari: Bado tunaishi katika dunia ya dhambi iliyojaa maumivu na mateso, na kila mmoja wetu hukabiliana na matatizo wakati fulani katika maisha, mambo yanayoweza kutufanya tuhoji upendo wa Mungu. Tunapotazama jinsi watu mbalimbali katika biblia walivyokabiliana na changamoto za maisha, tunaweza kupata ujasiri kwamba mwitikio wetu katika nyakati kama hizo unaweza kuimarisha safari yetu pamoja na Mungu, ambaye habadiliki (Malaki 3:6) na ambaye upendo Wake husalia kuwa thabiti.